Friday, September 11, 2015

UZURI WA MWANAMKE


UZURI WA MWANAMKE
















Mwanamke kwa kawaida ana sura tatu (3).


 (i) Sura ya nje (Reception)


(ii) Sura ya pili ya mwanamke mazingira ( tabia ,usafi wa nyumba nk)


(iii) Sura ya tatu ya mwanamke ni mfumo mzima wa uzazi mf uke na maeneo nyeti nk


Hii ndiyo sehemu nyeti na muhimu sana kwa mwanamke na ndio sehemu imemfanya
mwanamke aitwe mwanamke na apewe heshima sehemu hiyo pia inatakiwa kuwa safi muda wote. Lakini fikiria eneo hili wanawake wengi hawalithamini wala kulipa kipaumbele, na
ndio sababu imepelekea kusababisha matatizo makubwa ya kiafya katika eneo hilo. Hii huchangia matatizo makubwa kiafya ukianza na magonjwa kama UTI , muwasho, fangasi na matatizo mbalimbali yanayoenda mpaka kwenye kizazi na kusababisha matatizo makubwa baadae kama ugumba na kansa

Hebu jiulize swali; kama kweli kila siku unaweza kujicheki kwenye kioo mara kadhaa
kuhakikisha reception yako ya nje iko safi, na kila siku unafanya usafi nyumbani kwako
kuhakikisha mazingira ya nyumbani kwako ni safi na salama.


Je! Ni marangapi au ni lini umeweza kucheki afya yako ya ndani 


VIHATARISHI VYA AFYA YA SEHEMU NYETI NA


 UZAZI KWA UJUMLA


(i) Kuchangia nguo za ndani na vifaa vya kuogea, hii huwapata sana wanafunzi


(ii) Vyoo vya kuchangia (public toilets)


maofisini, maeneo ya soko, nyumba za ibada , sehemu za starehe,kwenye nyumba zetu tunakoishi nyumba za kupanga,vyuoni,mashuleni, nk.


(iii) Kutotumia maji safi na salama.


utakuta kuna ndoo ya maji chooni imeweka


 ukungu hujui maji yana muda gani usitumie 


kwani  maji haya hukaa bakteria hatari



 (iv) Matumizi ya pads za hedhi ambazo sio


salama.


wanawake wengi wanapomaliza hedhi huanza kutibu fangasi, michubuko, miunguzo, miwasho na vipele sehemu za siri.


(v) Bakteria
Bacteria hupatikana sehemu mbalimbali, unahitaji umakini katika matumizi ya vitu ktk sehemu za ndani.


Mfano unapofua nguo yako ya ndani unashauriwa kuanika juani au kupiga pasi kabla ya kuvaa.


 (vi) kutokufanya usafi ipasavyo kwa maeneo nyeti

   
  mwanamke ana miswaki 2 wa mdomoni na wa kikeni sukutua utoe siagi inayoganda kwa bibi ili kukuacha msafi  na kuondoa harufu mbaya.
sasa we dada unaefuga/kuunga kucha kidole cha kati hutaweza jisafisha vizuri na kama utaweza ina maana utajijeruhi kwa bibi na kusababisha vidonda kwani ngozi yake ni nyepesi sana. 
kumbuka unapokuwa na mpasuko wowote husababisha kupata m
aambukizi haraka sana.

Lakini pia jinsi ya kujisafisha unapopata choo kikubwa usithubutu kujisafisha kwa kutoa mkono nyuma kuleta kwa bibi kwani kinyesi kina bacteria hatari ambao watashambulia kwa bibi.


(vii) kufanya tendo la ndoa lisilo salama


CHUKUA TAHADHARI MAPEMA , KINGA NI BORA KULIKO TIBA.

Tuesday, August 18, 2015

KWANINI SASA HIVI WANAWAKE WENGI WANALEA WATOTO PEKE YAO (single mothers)

Kulea mtoto/watoto na mzazi mmoja ni tatizo kubwa sana katika jamii kama amefariki hiyo haina jinsi lakini kama wote mpo hai kuna athari wanapata watoto kama ya:-
1.  ukosefu wa maadili
2. ukosefu wa mahitaji ya msingi kwa mama asiye kazi ya maana.
3. ukosefu wa ushauri toka kwa baba
4. ukosefu wa maisha bora
tumeona watoto wangapi wapo na maisha magumu sana mpaka wanashindwa kwenda shule sababu mama hana uwezo.
wanakuwa wezi, watovu wa nidhamu na mabinti wanaanza mapenzi wakiwa wadogo sana ukiwauliza hali mbaya ya kiuchumi mama anashindwa kuwahudumia na inabidi akubali kusaidiwa na watoto, amabo kwa umri wao hawakustahili.

NINI KINASABABISHA KUWA SINGLE MOTHER

Nafikiri upande wa uvumilivu umekuwa mdogo kwa pande zote 2 yaani kwa baba na mama wa mtoto/watoto.
zamani bibi/mama zetu walikuwa wanavumilia mengi sana akiwa ananyonyesha basi hata amsikie mumewe ana mchepuko au aujue alikuwa hawezi kusema lolote kwa kuwa analea.
Na walikuwa wakivumilia visa na vituko vingi sana toka kwa waume zao ukimuuliza anasema hawezi kuondoka watoto bado wadogo wacha awalee wakue kwanza.

Na hata katika maisha yao kwa familia niliyotoka mie sijawahi kumsikia mama akihadithia uovu wa baba hata siku moja japo kwa shoga yake au kwa jirani.
Sio kwamba walikuwa hawakosani hapana lakini watoto tulikuwa hatujui saa ngapi wanagombana na saa ngapi wanapatana.

Salute kwa mama yetu katulea na mpaka sasa yupo na baba wana miaka 46 ya ndoa.

Wenza wa sasa hatuna maadili yaani ndoa zimekuwa ili mradi mmewaona viongozi wa dini ikapita dua basi lakini maisha mnayapeleka kama movie ya vichekesho.
Hakuna mwenye amri na mwingine akatekeleza wote mafahari ndani ya zizi moja lazima mmoja atoke.

Mdada ukiachana na mwenza wako  unatamba nitamlea mwanangu na nitamtunza kwa hali yoyote nisimuone kuja mtaka mtoto.  hizo huwa ni hasira na kutokuona mbele au kutothamini ubora wa mtoto.

Pia wadada mnadanganywa kubeba mimba kwanza ndio akuoe ili aonekane kidume basi kama ana uwezo kidogo ndio utajiachia na kumwamini kuliko Mungu aliyekuumba matokeo hakuoi unabaki kulea mtoto na sometimes na matumizi asilete.
unamwaminije mtu mliyekutana meno thelethini na ushee kinywani jamani ningewaona wa maana kama mngefunga hata mkataba kuwa asipokuoa umshitaki hivi hivi unaachia goli anafunga kweli?
ah wadada sometime akili zetu anajua aliyetuumba kwa kweli.
hebu tuvumilie kwa ajili ya watoto ili wakue katika malezi mazuri na bora wakijitegemea wanapunguza mzigo kwa wazazi kuliko wakikosa elimu wakawa na tabia za ajabu kila siku mama polisi kwenda kumtolea mtoto dhamana kashikwa kwa wizi au ukahaba.
turudi kwenye historia ya wazazi wetu ili tuokoe vizazi vyetu.
okay
am back baada ya kupata email, na sms nyiingi za kurudisha hii blog hatimaye nimekubaliana nanyi sasa mtaendelea kupata mada za mahusiano kama kawa.

kwa wale wapya karibuni sana humu ni mada za kujenga ndoa zenu itifaki inazingatiwa mtaelimik, mtaburudika  na mtafurahi yaah i promise that.
kwa mwenye maswali, maoni au ushauri kuhusu mahusiano naomba aulize kwa email, notification au sms.
kama litahusu jamii nitalijibu humu laa masuala ya binafsi nitamjibu private.
tupo katika kuelimishana na kukumbushana pale penye mapungufu
enjoy it
Johari Orig back again to you