Monday, February 17, 2014

Mpe raha mumeo kwa vyote

Habari za weekend wapendwa wasomaji wangu, pia za Valentine nadhani iliisha vyema kwa wale walioumizwa poleni sana,
maana kuna malalamiko nimetumiwa ya kila aina haki ya Mungu mapenzi siku hizi hakuna uuuwiiii,
wengine walizimiwa simu
wengine waliongopewa misiba, foleni, safari za ghafla duuh kwa ujumla poleni sana.
ukiona hivyo kura ya kui enjoy naye Valentine haikuwa yako subiri labda mwaka ujao kaazi kweli kweli.



Haya leo tuangazie ndoa zetu jamani 
Mke ni pambo ndani ya nyumba tena ni ua ridi linalonukia kwa kila aliye karibu nalo.
Ina maana mke unatakiwa ujipambe kwa tabia zilizo nzuri, umaridadi uvuke mipaka, huruma na mapenzi ya dhati visitengane kwa mumeo na familia yake kwa ujumla.

Hakikisha chumbani unatandika shuka kila baada ya siku mbili, fukiza udi, umepata maua ya yasmin, rose tupia ndani umekosa basi hata air fresh inayonukia vizuri pulizia ndani.
Kisha mwenyewe jipambe kwa lotion, pafyum au mafuta mazuri yenye harufu laini unajipaka wanja wako, poda bibi weye ili mradi sura iwe na mvuto akikuona uchovu wa kutwa nzima wote uishe ahisi faraja tena aone kachelewa haswaa kurudi nyumbani.

Baada ya usafi wa kina, maana wadogo zetu na wanetu siku hizi wananuka kwa bibi jamani, sijui malezi au ujuaji umewazidi?  Au ndio kuanza tiyari bado mapema? Wanaume wengi wanalalamika kwa hili, we mdada hasa unafuga au kuunga makucha mareefu unajisafisha vipi? 

Masikio machafu, mdomo tangu ulipopiga mswaki asubuhi mpaka kesho tena mmh, pua, kwapa, shingo kwenye pachi pachi zoote, nywele unaunga au unasukia nywele za bandia mwezi hadi  miwili bila kuzisafisha na joto la dar hili bichwa linanuka kama umefunika maiti ya panya,  mmmh wadada usafi wa haja unahitajika.

Kwenye mambo ya chakula cha usiku ndio kabisaaa, ujue uanamke wako hapo ndio unatakiwa uuonyeshe.
Haya ukiwa uwanjani mwenzetu ndio unalala tuu unasubiri ushikwe, uchokoze, basi hata kuinua mkono wako  ukapapasa kama kipofu washindwa heee weyee.  Ndio mwanamume huyo akitoka hapo hakutaki tena .

Lazima ujue mumeo/mpenzio anashikwa wapi akashikika, anapapaswa wapi akapapasika, anaguswa wapi akagusika hiyo ni shughuli yako mdada usidanganyike na porn ile ni biashara na sio asili yetu waafrika haswaa.   Sauti yako inatakiwa iwe nyororo yenye kudeka yenye kuchombeza kwa maneno mazuri, siyo wakati huo ndio uutumie kuomba pesa, au shida yako ulokuwa nayo, tunakosea.

ukishikwa onyesha kuhisi na akikuumiza sema hapo unaniumiza, kama unasikia raha sema ili ajue wapi akikushika unasisimkwa, sura iwe laini  macho yawe malegevu, akikutazama azidi kusisimkwa. 

Kulia hakukatazwi lakini kiwe cha kweli siyo makelele akikuangalia mwanaume macho makavu, sura umeikunja kama umelamba ndimu kelele nyiingi wizi mtupu. Hujihangaishi umetulia tuu zako kelele, hapana ule ni uwanja wa mashindano kati yenu kila mtu anatakiwa ajitume aonyeshe ujuzi jamani. Mwili wako ulainishe uunyumbuliishe kama huna mfupa, siyo unatulia kama unaombewa.

Tena mweleze kama umefika au bado hili ni tatizo la wanawake weengi sana hawafiki na wala hawafurahii tendo kwa sababu hawawi huru katika tendo yaani ili mradi atimize wajibu wake baasi.  Hapana unatakiwa kuongea na kujituma ili nawe ufike kileleni,  usipofika una hatari ya kuumwa kiuno kila mara.

Leo kama ameshinda mumeo kesho jitahidi manjonjo nawe umlize tena kwa kelele haswaaa.

Baada ya hapo kamuogeshe mumeo msinge, msafishe kwa mapenzi na huruma fyeka misitu yote abaki msafii.
Hakuna dawa zaidi ya hii tekeleza uone kama mumeo atachepuka.
Lazima abaki njia kuu.








Toa maoni yako

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako