Friday, January 24, 2014

MAANA YA MWANAMKE



Sam wa Dar

Dada mi nina tatizo naomba usipendelee kwa kuwa mwanamke mwenzio,
mke wangu hapendi kupika wala kazi za nyumbani kila kitu anafanya housemaid, hata kama usawa wenyewe basi unashindwa hatakutandika ndani mwako, ukimwelekeza ana mdomo mchafu balaa.  Naomba unisaidie bahati nzuri na humu kwenye blog yako anaingia 


JIBU

Mmmh aibu ulimtoa wapi au ndio mlikutana baa ukaona anafaa, 
Wahenga wanasema ni bora ukosee kujenga nyumba kuliko kukosea kuoa.

Haya nawe mwanamke mwenzetu ulilelewa mbinguni au chini ya bahari? Mwanamke kutokujua kupika shost majanga tena  tukushushie bendera nusu mlingoti, we ni wa kike sio mwanamke, mwanamke hawezi kuwa hajui kupika, na kitanda utandikiwe khaaaa.

Nyie ndio mnaosababisha wasaidizi wanabakwa/wanabebeshwa mimba na waume zenu kisha mnawafukuza kwa taadhira, wanaenda makwao kuongeza mzigo wa umasikini, kumbe kosa lako mwenyewe.

Fahari ya mwanamke ndani ya nyumba usafi uujue, chakula cha mumeo bibi weye, chumbani  kwako ndio kabisa huyo maid hatakiwi hata kuchungulia, ukiambiwa mdomo na ndivyo walivyo wavivu wote mdomo silaha, waongo, chochote kwao sawa tuu,  kazi ni kuunga kucha na kuzitia kila aina ya  rangi sijui hata usafi wa maungo yao wanaufanyaje.

Kila siku unazusha safari ili usikae jikoni, saluni zote wanakufahamu aliyekwambia mwanaume anakula urembo nani, mapenzi sio kitandani tuu bali umjue mwanaume kula yake, vaa yake, apendavyo ufanye na anachokukataza acha, pia uwe mbunifu basi ndani ya nyumba kila mara unatakiwa um surprise mumeo kwa upambaji wa nyumba yenu. Badilika my dear maisha si lelemama hapo ulipo kuna wenzio wamepanga msitari  wanakusubiri utoke waingie.

Asikudanye mtu maisha ya ndoa yana heshima kwako na nyumbani kwenu.  Kama hufahamu kuwa mpole tafuta mtu japo umlipe akufundishe wajibu wa mwanamke  vinginevyo utawahesabu wanaume kama nguo.

Kila kitu msaidizi siku ukimkuta anakusaidia kitandani usihamaki kachukue pop corn  uangalie tv sebuleni uache muvi iendelee.
MAANA YA MWANAMKE NYUMBA

Bye

















Toa maoni yako

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako