KWA NINI TUNAPENDA?
Kwanza kabisa tuelewane kuwa kuna kupenda na kutamani
KUTAMANI
NI kumtamani mtu kwa ajili ya tendo yaani unakuwa na hamu ya kufanya nae ngono kisha baada ya hapo utakuwa unamtafuta pindi utapopata hamu tena.
Na hii ina madhara makubwa sana kuliko faida, hasa kwa wanawake wa kiafrika.
Kwanini?
kwa sababu wanawake wa kiafrika hasa wa Kitanzania maadili na mwenendo wao mwanamke hata awe mzuri hutegemea atongozwe na mwanaume.
Sasa kiakili hasa ambao wapo kwenye foolish age huona raha sana kutongozwa na hata huweza ongea mbele ya wenzake kuwa ametongozwa na fulani.
Bila kuwa mwangalifu hukubali kuingia kwenye mahusiano bila kufikiria mara mbili na hasa kama aliyemtongoza atakuwa na uwezo, maarufu au mzuri, ndio kabisa.
Bila kuchunguza kama huyu mtu alikuwa anamtamani na sio kumpenda.
UTAJUAJE KAMA HUYU MWANAUME ANAKUTAMANI?
1. Hajali kujua mambo yako yaani mwonekano wako katika jamii
2. anakupa sifa zingine hata huna
3. huwa na pupa ya kutaka tendo la ngono kila mnapokutana na si maongezi mengine
4. hajali mawasiliano yako yaani kama simu akupigie yeye wewe ukipiga anaweza asipokee.
5. hana adabu katika maongezi na mbele za watu hutaka kujionyesha kuwa yeye mpenzi wako.
Ni baadhi tu ya dalili za mwanaume anayemtamani mwanamke.
FAIDA
hakuna faida kwa mwanaume kama huyu zaidi ya kujeruhi moyo wako
MADHARA
ni makubwa sana tena yanaharibu mfumo mzima wa vizazi vijavyo na Taifa kwa ujumla
Baada ya tendo la ngono:-
1. Sifa alizokuwa anakupa, we mzuri na nini vinakata
2. Majina mara baby, honey, sweetheart yanakufa utaitwa jina ulilopewa na wazazi wako.
3. Mawasiliano ya mara kwa mara yanapungua na sababu nipo busy, mikutano, safari
visingizio viingi.
4. Kama alikuwa anakutoa out zinapungua kama sio kwisha kabisa, na kama ulikuwa unapewa
pesa ya taksi sasa utaambiwa kopa atalipa wakati hatalipa, au panda dala dala.
5. kama ulitoa shida basi kutakuwa na visingizio visivyokuwa na idadi
6. Ole wako umwambie una mimba majibu yake yatakuwa hivi:-
a. Wee nani kakwambia kubeba ndio tulivyokubaliana ah utajua mwenyewe na ole wako unitaje.
b. Hapana sio yangu mtu mwenyewe una mabwana chungu nzima unadhani sijui, habari zako
zote ninazo.
c. Mmmh basi tuitoe bwana mi si unajua nina mke nyumbani sasa unadhani akijua itakuwaje.
d. Ah basi nitaitunza lakini usinitaje iwe siri yetu
na mengine mengi majibu yasiyo na mwelekeo ukiona hivyo ujue imekula kwako.
MATOKEO YAKE
- unaathirika kisaikolojia na kuwachukia wanaume wote duniani
- magonjwa ya zinaa, ukimwi n.k
- kama utazaa mtoto pia nae hatakuwa na furaha kama watoto wenzie wenye baba na mama.
- hatakuwa na matunzo bora kama mama huna uwezo
- hatasoma vizuri na wengi huishia la saba.
- kama mtoto wa kike mara nyingi nae huishia kuzalishwa akiwa na umri mdogo.
- umasikini unakuwa kwa kasi ya ajabu.
- Taifa linakosa nguvu kazi.
haya na mengine mengi sana ambayo yanawakuta wanawake kwa jambo moja tu KUTAMANI
Tuonane tena msomaji hapa hapa
`
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako