MAPENZI NI NINI
Kwa haraka haraka ukiulizwa mapenzi ni nini utajibu ni wawili wapendanao kitu ambacho sio kweli
ingekuwa kweli wapendanao wasingekuja kuachana.
Ukweli ni kwamba, mapenzi ni maumbile yana roho yanatembea na kuishi kama alivyo mwanadamu.
KWANINI?
Kwa sababu jiulize umependa mara ngapi ukaumizwa mara ngapi na iliapa mara ngapi kuwa hutopenda tena na ukarudi ukapenda.
Na wakati unapenda unakuwa kama mtu ambaye unaishi maisha ya raha ya pekee ambayo unadhani hakuna yeyote dunia hii anaefaidi mapenzi kama wewe.
na ukitendwa unaiona dunia haifai, hakuna raha duniani, aliyekutenda unamuona adui wa maisha yako, ukiona watu wanapendana unawaona wajinga na kuwafikiria nao watayapata yaliokukuta wewe.
Ndani ya moyo wako utajuta na kusononeka kwanini ulipenda, kwanini ulitumia muda wako na pesa pengine katika kudumisha mapenzi yako. na hupelekea mpaka ukaapa kuwa hutopenda tena na kuwaonya watu kuhusu kuendekeza mapenzi.
Je ni kweli hutopenda tena?
tuonane hapa hapa
mmh ni kweli wanawake wengi wameathirika kutokana na kuamini wanaume hovyo, akiambiwa tu nakupenda baaaass
ReplyDelete