Leo tuongelee upande wa waume zetu.
Mwanaume nyumbani kwako ndio mahali pa faraja umetoka
kuhangaika machovu ya kazini unapozea home kwa kuiona familia yako ipo salama
wamekula, unapanga nao mikakati ya kesho, sio unakuwa mkali kama pili pili,
mkeo na watoto wakikuona wanachanganyikiwa.
Mwanaume unaandaliwa kila kitu kuanzia mavazi, chakula, maji
ya kuoga na vinginevyo, kumwambia mkeo ahsante washindwa.
Mwanaume unatoka kwenda kazini hata busu kwa mkeo hakuna, ile
kumuaga tuu mwenzio shida.
Unarudi kazini ukifika nyumbani mkeo anakupokea kwa furaha
na bashasha basi hata kutabasamu na kumuonyesha furaha mkeo hakuna zaidi ya
kuitika kwa kichwa au mmmh. Wakati mwenzio alikuwa hana raha anawaza utarejea
saa ngapi ili awe nawe.
Mnakaa sebuleni kama mtu na mkwewe kila mtu kochi lake, basi
we jicho kwenye tv tena channel
unayotaka, maongezi na mkeo huna zaidi ya kumuuliza kama chakula tayari, na
mnapokula kimya kama maadui hata kumsifia mkeo kama chakula kizuri inashindikana,
basi kama kazidisha chumvi kidogo ndio utamgomba kama mtoto.
Ukitoka hapo unapanda kitandani kimya unamwacha mkeo kwenye
wakati mgumu, hajui leo utakula chakula cha usiku ama laa. Basi masikini mwanamke huyu baada ya kumaliza
shughuli zake za kukuandalia mavazi yako viatu abrash mwenyewe atapanda kitandani
kimya kimya, ole wake akutupie hata mkono unautupa “mi nimechoka bwana”. Na hata kama ukikitaka basi
hakuna maneno mazuri zaidi ya mkono kumpelekea kuwa akae tayari maana we ndio
unataka.
Ndani mwenu upate muda wa kucheza na mpenzio/mkeo utani
kidogo sio kila wakati we busy na simu au magazeti mkeo akikusemesha unamjibu
kwa karaha.
Kama unavuta sigara ndio utapanda nazo hadi kitandani bila
kujali mwenzio anaichukuliaje harufu ya sigara.
Mkeo/mpenzio akikosea basi utamsema chumbani ambako ni nyie wawili tuu ndio
mnaokitumia, sio kumsema mbele ya
familia au hata mbele za watu mpaka
anajiona hafai kuitwa mwanadamu.
Matendo haya hata kama mkeo anakupenda namna gani hatakuwa
na furaha maishani mwake, ile akikuona tu basi roho yake inamwenda mbio kama
kaona simba.
Ukitoka hatamani urudi na ukirudi anaomba usiku uche ili
uondoke.
Haya ndio niliyoyaona kwenye maswali ya wanawake wengi.
Toa maoni yako
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako