Friday, February 7, 2014

MNAOJIANDAA NA VALENTINE-NGONO MNAYAJUA HAYA?

Valentine hiyooo inakuja   wake/waume za watu roho juu, 


Watu ndio wameanza booking mapema, tena karibu asilimia 75 ni wapenzi tuu sio wa ndoa tena usikute mke wa mtu au mume wa mtu. 

Haya kuna kipya kipi wenzetu mnaenda kukifanya ambacho kitawafanya baada ya hapo mfunge ndoa?  Kabla ya hapo hamkuwa na mapenzi ya kutoka pamoja?

Au wewe mke wa mtu/mume wa mtu mapenzi gani utaenda onyesha huko wakati umeshindwa kuonyesha mapenzi hayo nyumbani kwako.

Kwanza kwa wadada, 
Kupendwa na mume/mke wa mtu ni adhabu sana kwani akipigiwa simu na mumewe/mkewe inabidi unyamaze kimya wadanganyanee I love you makiss meengi umetulia kweli? 

Pia ni mwongo mkubwa kama anamuongopea aliyemuoa mbele ya viongozi wa dini au serikali akaapa kumtunza kwa raha na shida wewe atakuambia ukweli gani? 

Na wewe kaka una mke wa mtu tena anathubutu hata kukuletea pesa unachekelea, akiachwa utamuoa kweli?  Hujiulizi kama mwanaume mwenzio anamfanyia hayo kwako wewe ndio atakuwa mke mwaminifu?

Anapigiwa simu na mumewe anadanganya na wewe unachekelea na kumuuliza anasemaje huyo bwege,
bwege wewe unaetembea na mwanamke ambaye huna future naye.

Hebu zinduka dada/kaka unaependwa na mume/mke wa mtu halafu anakudanganya anakupenda yule wala hana shida nae mbona hamwambii kwenye simu kama yuko na wewe, mbona hamwachi akawa na wewe. 

Hakuna moyo unaopenda wawili kwa wewe kaka mume wa mtu una mkeo home umekazana kuchezea mioyo ya wadada, mkeo anakupenda anakupa kila upendacho amekuzalia watoto wazuri badala ya kutunza familia yako umekazana na wadada wa mjini unawaona wazuri hujui hata aliyewafanya wawe wazuri nani.

Unaingia kichwa kichwa mpaka familia yako unaiweka katika hali mbaya, wakati hivyo unavyotunza huko nje ungemtunza mkeo angependeza kuliko na huyo mnaekutana mchana usiku hujui kalala na nani.

Valentine ina maana gani kwenu, upendo gani wa siku moja kisha kila mtu anarudi kwake.  Tena kuna wengine anapaga guest kuanzia asubuhi mpaka jioni ana wapenzi watatu mpaka wanne. Mwenyewe anajisifu kweli kweli kala valentine vizuri wakati alikuwa gari la taka umezoa kwa wote kisha unaenda kutupa kwa mkeo masikini hana hili wala lile anaambulia magonjwa.

 Tumuogope Mungu jamani kuwauwa bila sababu wake/waume zetu.

Wengine wanatongozana eti siku ya valentine wakaanze ngono jamani upendo gani sasa mnaoenda kuuonyesha na ndio kwanza mnaanza baada ya valentine mapenzi chali, kila mwaka uta valentine na mpenzi mpya.
Ushauri wangu hasa nyie wakaka tafadhalini siku hiyo mchukue mkeo mpeleke hoteli nzuri ale, anywe, ikibidi hata kulala mna show  love usiku kucha  unampoza machovu ya kukufanya uwe handsome boy mjini.

Asubuhi mnarudi home taratiiiibu hadi raha wenyewe mmeshikana mikono hata Mungu hutia Baraka ndoa yenu.
Msiokuwa couple  si lazima ungonoke show love kwa mama, dada au mtu yeyote aliye rohoni mwako basi kama huna shinda kwenye mitandao uwe una like na ku comment mpaka usiku kwani utakufa.

Ni hayo tuu wapendwa kwa wapenda ukweli 








Toa maoni yako

No comments:

Post a Comment

Toa maoni yako