Watu ndio wameanza booking
mapema, tena karibu asilimia 75 ni wapenzi tuu sio wa ndoa tena usikute mke wa mtu au mume
wa mtu.
Haya kuna kipya kipi wenzetu mnaenda kukifanya ambacho
kitawafanya baada ya hapo mfunge ndoa? Kabla
ya hapo hamkuwa na mapenzi ya kutoka pamoja?
Au wewe mke wa
mtu/mume wa mtu mapenzi gani utaenda onyesha huko wakati umeshindwa kuonyesha mapenzi hayo nyumbani kwako.
Kwanza kwa wadada,
Kupendwa na mume/mke wa mtu ni adhabu sana kwani
akipigiwa simu na mumewe/mkewe inabidi unyamaze kimya wadanganyanee I love you
makiss meengi umetulia kweli?
Pia ni
mwongo mkubwa kama anamuongopea aliyemuoa mbele ya viongozi wa dini au serikali akaapa kumtunza kwa raha na shida wewe atakuambia ukweli gani?
Na wewe kaka una mke wa mtu tena anathubutu hata kukuletea pesa unachekelea, akiachwa utamuoa kweli? Hujiulizi kama mwanaume mwenzio anamfanyia hayo kwako wewe ndio atakuwa mke mwaminifu?
Anapigiwa simu na mumewe anadanganya na wewe unachekelea na kumuuliza anasemaje huyo bwege,
bwege wewe unaetembea na mwanamke ambaye huna future naye.
Hebu zinduka dada/kaka unaependwa na mume/mke wa mtu halafu
anakudanganya anakupenda yule wala hana shida nae mbona hamwambii kwenye simu
kama yuko na wewe, mbona hamwachi akawa na wewe.
Hakuna moyo unaopenda wawili kwa wewe kaka mume wa mtu una
mkeo home umekazana kuchezea mioyo ya wadada, mkeo anakupenda anakupa kila
upendacho amekuzalia watoto wazuri badala ya kutunza familia yako umekazana na
wadada wa mjini unawaona wazuri hujui hata aliyewafanya wawe wazuri nani.
Unaingia kichwa kichwa mpaka familia yako unaiweka katika
hali mbaya, wakati hivyo unavyotunza huko nje ungemtunza mkeo angependeza
kuliko na huyo mnaekutana mchana usiku hujui kalala na nani.
Valentine ina maana gani kwenu, upendo gani wa siku moja
kisha kila mtu anarudi kwake. Tena kuna
wengine anapaga guest kuanzia asubuhi mpaka jioni ana wapenzi watatu mpaka wanne.
Mwenyewe anajisifu kweli kweli kala valentine vizuri wakati alikuwa gari la
taka umezoa kwa wote kisha unaenda kutupa kwa mkeo masikini hana hili wala lile
anaambulia magonjwa.
Tumuogope Mungu
jamani kuwauwa bila sababu wake/waume zetu.
Wengine wanatongozana eti siku ya valentine wakaanze ngono
jamani upendo gani sasa mnaoenda kuuonyesha na ndio kwanza mnaanza baada ya
valentine mapenzi chali, kila mwaka uta valentine na mpenzi mpya.
Ushauri wangu hasa nyie wakaka tafadhalini siku hiyo mchukue
mkeo mpeleke hoteli nzuri ale, anywe, ikibidi hata kulala mna show love usiku kucha unampoza machovu ya kukufanya uwe
handsome boy mjini.
Asubuhi mnarudi home taratiiiibu hadi raha wenyewe
mmeshikana mikono hata Mungu hutia Baraka ndoa yenu.
Msiokuwa couple si
lazima ungonoke show love kwa mama, dada au mtu yeyote aliye rohoni mwako basi
kama huna shinda kwenye mitandao uwe una like na ku comment mpaka usiku kwani
utakufa.
Ni hayo tuu wapendwa kwa wapenda ukweli
Toa maoni yako
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako