Nimepata maswali ya wasomaji weengi zaidi ya 20 wanalalamika kuhusu usaliti wa wapenzi wao naomba niwajibu kwa pamoja ili nipunguze foleni ya maswali yenu:
Kwanza kama ulisoma mada yangu ya TALK ABOUT LOVE yote utapata majibu mazuri zaidi lakini naomba nijibu tena.
Suala la mume/mke/mpenzi wako kukusaliti inatokana na mambo mengi sana haya ni baadhi tu:
Anakupenda kweli?
Maana huenda alikupenda ajili ya kitu fulani mfano mwanaume alikupenda ulikuwa na sura nzuri, umbo namba 8 sasa umejiachia kunenepa mpaka hata alivyokupendea vimetoweka, au ajali masikini umepoteza kiungo au sura imeharibika.
Kwa mwanamke huenda ulikuwa na mali, Umaarufu au umbo zuri baadaye vikatoweka.
Anayekupenda kweli hakusaliti hata ufikwe na majanga gani.
- Kauli mbovu
- Chakula cha usiku
Kwa mwanamke ukiona mumeo anakunyima muulize vizuri kama hujamkosea jua kuna mwenzio anamchosha maana huwa hawawezi kuvumilia bila hiyo kitu.
Au we dada unaefanya kazi ukianza kwenda kazini unajipara kweli kweli, ukirudi unatafuta kanguo hakana hata sura ndio unavaa we unadhani mumeo anaona waliojipara wangapi huko nje. Na hizo nguo na vipodozi alivyonunua aishie kuona unajipara wakati unatoka inaingia akilini kweli.
Pia usafi wa kwa bibi jamani tuseme ukweli kuna wadada wengine wananuka sana, kwa sababu hawapendi kutumia maji kujisafisha, mwanamke maji ndio kila kitu, pia usisahau mwanamke ana miswaki miwili, kujipara usoni hakuna maana kama hujisafishi vizuri, hamu yote humuisha mwanaume akikuta kwa bibi kuna uvundo shost, atakupa mgongo kama hakujui.
Na nyie wanaume mabahili, mkeo hajui mapato yako, humpi chakula kizuri, mavazi anayaona yanang'aa kwenye maduka, kila siku unamwimbia wimbo wa subira, dagaa lake mchicha ndio kabisa kila siku, pesa ya matumizi unampa kila siku haitoshi hata mlo wa siku, mwanamke hana hata akiba kidogo haaa weee akimpata anayempa elf kumi tu atakusaliti lazima.
- Makaribisho mabovu
- Usafi/umaridadi
Au we dada unaefanya kazi ukianza kwenda kazini unajipara kweli kweli, ukirudi unatafuta kanguo hakana hata sura ndio unavaa we unadhani mumeo anaona waliojipara wangapi huko nje. Na hizo nguo na vipodozi alivyonunua aishie kuona unajipara wakati unatoka inaingia akilini kweli.
Pia usafi wa kwa bibi jamani tuseme ukweli kuna wadada wengine wananuka sana, kwa sababu hawapendi kutumia maji kujisafisha, mwanamke maji ndio kila kitu, pia usisahau mwanamke ana miswaki miwili, kujipara usoni hakuna maana kama hujisafishi vizuri, hamu yote humuisha mwanaume akikuta kwa bibi kuna uvundo shost, atakupa mgongo kama hakujui.
- Matumizi
Na nyie wanaume mabahili, mkeo hajui mapato yako, humpi chakula kizuri, mavazi anayaona yanang'aa kwenye maduka, kila siku unamwimbia wimbo wa subira, dagaa lake mchicha ndio kabisa kila siku, pesa ya matumizi unampa kila siku haitoshi hata mlo wa siku, mwanamke hana hata akiba kidogo haaa weee akimpata anayempa elf kumi tu atakusaliti lazima.
- Ugomvi wa kila mara
Ndio unakuta mwanaume akitoka kazini anakaa kwanza mahali mpaka saa nne za usiku ndio unarudi na kusingizia foleni, lakini ukweli haoni faida ya kurudi home mapema atamaliza siku vibaya. akimpata wa kumpa raha na sio karaha zako atasahau hadi jina lako.
Jamani usaliti unaumiza sana kama msumari wa moto kwenye kidonda
Tafadhali usimsaliti mwenzio
Toa maoni yako
Toa maoni yako
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako