Napenda kuungana na Wazanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya MAPINDUZI YA ZANZIBAR
Leo naomba niwape vitu vya Zanzibar ambavyo sehemu nyingine ni adimu kuvipata.
Kwanza wazanzibari ni wakarimu na waaminifu sana ukipata tatizo hukuhudumia kama mnajuana tangu zamani.
- USAFIRI
Usafiri wa kuingia na kutoka Zanzibar ni wa anga na bahari tuu
Katika Tanzania nzima hakuna sehemu wanawake wanavaa mavazi ya aina moja kama Zanzibar inapelekea hata wageni kuiga mavazi ya kujistiri mwili. wenyewe huitwa utamaduni wa mzanzibari.- SITTING ROOM
wazanzibar hupenda kuweka mazuria na mito tu hivyo kama hujui kukunja miguu utaondoka kabla ya wakati.
Hotel iliyoko katikati ya bahari inasemekana ni hotel ya kwanza duniani.
- DORIAN
hili tunda linanuka sana kiasi ukilibeba popote ukipita lazima watu wajue kama unalo, lakini ni tamu sana wenyewe hula hata kwenye chakula, wengine wakimaliza kulila hupiga mswaki.
wageni wakifurahia vyakula Forodhani
- FORODHANI
Hii ni sehemu nzuri sana katika Tanzania hakuna mahali pazuri kama hapa
kuna vyakula vingi vya kizanzibari vitamu,
hapachagui mwenye nacho au hana
hapana kiingilio wala hulazimishwi kununua
huenda kila rika hapachagui wazee, vijana au watoto, wageni au wenyeji
wazanzibari hutumia sana mahali hapa kubarizi au kupunga upepo baada ya pilika za kutwa nzima.
Haya haya hivi ni baadhi ya vitu nilipenda nawe uvielewe.
MAPINDUZIIIIIIIIIIIII
DAIMAAAAAAAA
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako