Tuesday, January 21, 2014
MASWALI YENU - TALK ABOUT LOVE
Assalaam alaykum
Samahani kwa kuto onekana kwa sababu ambazo zilikuwa nje ya uwezo wangu.
Leo nitawaletea maswali ya wasomaji wangu kama walivyoniandikia, ila itifaki itazingatiwa sitatoa picha wala address ya muhusika bali jina la mwanzo tuu.
Jane wa Arusha:
Habari dada mimi nimefuatilia sana mada yako humu nimepata uelewa sana ahsante dada Mungu akubariki. Sasa swali langu linakuja hivi
mimi nina mume wangu tuna miaka 3 hajawahi kuniridhisha kimapenzi na wala hajali akimaliza yeye basi anaendelea na mambo mengine au kama ni usiku anakoroma dada nifanyeje?
Jibu
Tatizo hili lipo wanawake wengi wanalalamika, wengine wanafikia hata kutoka nje ya ndoa zao jamani sijui kwanini baadhi ya wanaume ni wabinafsi sana wakisharidhika basi utafikiri alikuwa na toy.
Jamani wanaume mnaopitia humu jiangalieni sometime mnavunja mapenzi na ndoa zenu wenyewe, mwanamke atakupendaje wakati humridhishi acheni mfumo dume.
Kwanza sijafahamu ilikuwaje mpaka kufikia hatua ya kufunga ndoa, pili hujaniambia umri wako ni miaka mingapi,
Kama mlianza mapenzi kabla ya kufunga ndoa ina maana hilo suala hukulipa umuhimu, kwa sababu tamu ya chai sukari, kama mwanaume ni mbinafsi kitandani wa nini sasa. Utaishije ndani ya ndoa bila kufurahia tendo wakati ndilo linalomfanya mtu apende kupita kiasi.
Pia wakati wa tendo unatakiwa mawazo yako uyahudhurishe hapo na uhisi kila tendo analokufanyia mpenzi/mume wako linakufurahisha, kama kuna sehemu akikushika unahisi raha basi ni vyema kumwambia, au anakuumiza pia sema ili uweze kufurahia. Na kama bado hujawa tayari mwambie we bado hujakiona kituo. Pia maandalizi yawe mazuri unayofurahia sio anakoshika siko unakojisikia na akitaka kufanya haraka we macho makavu mwambie aendelee na romance kwani hakuna raha kama hujalewa na romance maana utachunika na kulichukia tendo. Matokeo yake utakuwa unamtazama jicho kali sura umeikunja kama uko vitani. haaahaaa inakuwa kashda tena, ukitoka hapo umeumia kama umebakwa.
Pia je msitu umefyeka? kwa wote wawili maana kama mmoja wenu anao mmh shost msitu unakata kuliko wembe hivyo ni muhimu sana kusafisha msitu
Jambo lingine umri kisaikolojia mwanamke kuzama kwenye mapenzi, kujua thamani ya penzi, akahisi raha, umakini, akafurahia tendo, akalia ki kweli kweli kwa raha ni kuanzia miaka 30-35 na kuendelea iwapo atakuwa na mwanaume anaye yajua mapenzi haswaaaa.
Vinginevyo mmh.
Ok tuonane kwa swali jingine
Tchao
Toa maoni yako
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment
Toa maoni yako